Arne Slot anayataka makombe yote msimu huu

Liverpool imefuzu kucheza hatua ya robo fainali ya kombe la Carabao  imejikusanyia alama 9 kwenye ligi ya mabingwa baada ya kushinda michezo yake mitatu na inashika nafasi ya pili EPL nyuma ya Manchester City ikiwa imejikusanyia  alama 22.

Kocha wa Liverpool Arne Slot ameweka wazi tamaa aliyokuwa nayo ya kushinda ubingwa wa mkombe yote ambayo timu yake inashiriki msimu huu wa 2024-2025. Slot ameyasema hayo alipokuwa kwenye mkutano wa Waandishi wa habari kuzungumzia mchezo wa EPL utakaochezwa Novembe 2 Anfield.

Pages

Subscribe to East Africa Television RSS