Ruben Amorim kutangazwa muda wowote Man United

Ruud van Nistelrooy atakiongoza kikosi cha Mashetani Wekundu katika mchezo wa ligi siku ya kesho Jumatano dhidi ya Leicester City, huku klabu ikisubiri kumtambulisha Kocha mkuu muda wowote kuanzia siku ya  kesho. 

Klabu ya Sporting Lisbon imetoa tamko kuhusiana na klabu ya  Manchester United  kukubali  kulipa kiasi cha fedha  bilioni 17 za Kitanzania ili kuweza kupata huduma ya Kocha wao Ruben Amorim ambaye anahitajika na klabu hiyo ya Uingereza kuchukua nafasi ya Erik Ten Hag  waliyemfuta kazi jana

Pages

Subscribe to East Africa Television RSS