Polisi nchini Kenya yawasaka Al-shabaab
Polisi nchini Kenya imeimarisha operesheni za usalama katika mji wa Mandera uliopo mkoa wa Kaskazini Mashariki mwa Kenya, na kuwasaka wapiganaji wa al-Shabaab waliovamia misikiti miwili na baadaye kutoa hotuba mbele ya waumini waliomo ndani kabla ya kuondoka.