
Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Kaskazini Mashariki George Seda amesema, wapiganaji hao walibeba bunduki aina ya AK47 na kwenda kwenye misikiti ya Elram A na B wakati wa sala ya alfajiri Jumamosi na kuwaambia waumini waliokuwepo misikitini kuwa wapo kwenye vita na watu wasio waislamu na kuwataka wajiunge na vita hivyo. Kwa mujibu wa Seda hakuna aliyejeruhiwa kwenye tukio hilo.
Habari nyingine zinasema, huko nchini Somalia limetokea shambulio la gari lililotegwa mabomu ambalo lililenga hoteli maarufu katika mji wa Kismayo uliopo kusini mwa nchi hiyo siku ya Jumapili.