Barcelona yatibua rekodi ya Real Madrid

Usiku wa jana Oktoba 26, 2024 kwenye uwanja wa Santiago Bernabeu ulichezwa mchezo wa El Clasico klabu ya Real Madrid iliikaribisha klabu ya mpira wa miguu ya Barcelona katika  muendelezo wa michezo ya ligi kuu nchini Hispania La liga.

Kabla ya mchezo wa jana El Clasico kuchezwa Mabingwa watetezi wa La liga Los Brancos ilikuwa inapambania  rekodi ya kucheza michezo 43 bila kupoteza rekodi ambayo ilikuwa inashikiliwa na Barcelona ya kucheza michezo 43 bila kupoteza kuanzia 2017-2018.

Pages

Subscribe to East Africa Television RSS