Nyota wa Golden State Warriors Stephen Curry amepata majeraha timu yake ikipoteza dhidi ya Los Angeles Clippers kwa alama 112-104. Curry alipata majeraha kwenye mchezo wa ligi ya kikapu nchini Marekani maarufu NBA dhidi ya Clippers mchezo uliochezwa jana Jumapili Oktoba 27, uwanja wa Chase Center.
Stephen amewahi kushinda tuzo ya MVP mara mbili amekuwa na historia ya kuumia kifundo cha mguu wake mara kwa mara amefunga alama 18 huku Warriors ikipoteza mchezo wake wa kwanza wa NBA msimu huu.