Wavuvi wamlilia Rais, fidia ya oparesheni Sangara.
Wavuvi kanda ya ziwa wamemwangukia Makamu mwenyekiti wa CCM bara Abrahman Kinana na kumuomba kufikisha kilio chao kwa Rais kuhusu tatizo la uvuvi haramu na kuomba kulipwa fidia kutokana na oparesheni sangara ya mwaka 2018 iliyofanywa dhidi yao ambayo ilileta hasara ya fedha nyingi.