Miguel Gamondi alalamikia ratiba inabana timu yake

Kocha mkuu wa Klabu ya Yanga Miguel Gamondi amesema ratiba ya Ligi Kuu ni ngumu kutokana na ukaribu wa michezo. Gamondi ameeleza hayo wakati mkutano na Waandishi wa habari kuelekea mchezo dhidi ya Coastal Unioni hapo kesho Oktoba 26 Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Arusha.

Timu ya Wanachi inashika ya pili nyuma ya Singida Black Stars ikiwa imejikusanyia alama 18 katika michezo sita iliyocheza imefunga goli kumi na moja na haijaruhusu goli mpaka sasa kwenye ligi kuu ya Tanzania bara TPL.

Pages

Subscribe to East Africa Television RSS