Watu watano wafariki kwenye ajali Shinyanga
Basi la Kampuni ya Super Najmunisa lililokuwa likitoka Jijini Dar es salaam kuelekea Mkoani Mwanza limegongana uso kwa uso na Fuso katika eneo la Ibadakuli Manispaa ya Shinyanga na kusababisha vifo vya watu watano na majeruhi 56.