Wanawake 8 wauawa Masasi yupo aliyepigwa mawe
Wanawake nane wameuawa kwa nyakati tofauti katika wilaya ya Masasi mkoani Mtwara kwa kipindi cha kuanzia Machi hadi Agosti mwaka huu, akiwamo mwalimu wa shule ya msingi Mbanju ambaye aliuawa kwa kupigwa mawe, huku mapenzi na ugomvi wa mali ukitajwa kama chanzo cha mauaji hayo.