Sabaya afanyiwa upasuaji wa kichwa
Kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya, imeahirishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi mjini Moshi, kwa kile kilichoelezwa mahakamani kwamba mshtakiwa wa kwanza Lengai Ole Sabaya, amefanyiwa upasuaji wa kichwa.