Watoto watatu watelekezwa na wazazi wao
Mkuu wa wilaya ya Ulanga mkoani Morogoro, Ngollo Malenya, ameagiza kukamatwa kwa wazazi wawili Thomas Ulanda na Adelyda Nakashawa, baada ya kuwatelekeza watoto wao watatu wanaoishi Kijiji cha Gombe, huku mmoja ambaye ni wa kidato cha nne akipambana kuwahudumia wadogo zake.