Tutafanya mabadiliko makubwa - Rais Samia
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameunda Kamati ya watu 12 na Sekretarieti ya watu watano kwa ajili ya kumshauri njia bora za kuleta mabadiliko ya utendaji kazi wa haki kwenye vyombo vya haki jinai nchini.