PRESENTERS

TONY ALBERT
+
TONY ALBERT

Amezaliwa Tarehe 10/06 Mwanza na kukulia ndani ya jiji la Dar es Salaam.Amesoma shule za Esaacs Primary School na Kampala International High School.
Tbway ana urefu wa futi 6.5 . Anapenda sana kupiga picha, kuogelea, movie na kuendesha magari kwa kasi. Alipachikwa jina la TBWAY 360 akiwa na umri wa miaka 14 baada ya kuzungusha gari mzunguko wa duara yaani nyuzi 360

MAGGIE VAMPIRE
+
MAGGIE VAMPIRE

Nimeshiriki miss universe mwaka 2011 mara baada ya kumaliza chuo  na kufanikiwa kuingia katika Top finalist.

Vilevile mwaka uliyofuata nilishiriki  miss Tanzania na kufanikiwa kushinda taji dogo la top Model (fast track)

na pia kufika hatua za juu za miss Tanzania top 5 finalist 2012.

Napendelea kufanya mazoezi, kuogelea, kucheza mziki, kusafiri, kukutana na marafiki wapya ili kubadilishana mawazo,

Napendelea pia kuangalia Cinema mbali mbali na kujifunza vitu vipya.

Sponsored BY

JUDGES

ARTICLES

"Ubunifu katika mashindano", moja kati ya makundi yaliyojitokeza 'The Quest Crew' wakiwa wamevaa kininja.

8 Aug . 2015

Makundi yaliyofanikiwa kuingia robo fainali kutokea hapa Don Bosco Upanga katika mashindano ya #2015Dance100

1 Aug . 2015

Moja ya makundi, Mavuno Crew wakionyesha uwezo wao mbele ya majaji katika michuano ya usahili wa pili leo

1 Aug . 2015

usahili wa kwanza Dance100%2015 uliofanyika TMK jijini Dar es Salaam

26 Jul . 2015

Dance 100%

4 Jul . 2015

Pages

Dance 100% ni shindano la nguvu kinoma ambalo huandaliwa na kituo cha television cha EATV na hufanyika kila mwaka kwa muda maalum uliopangwa.

Shindano hili lipo kimtaani zaidi, maana hutembelea mitaa mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam na kuweka vituo vyake kwaajili ya kufanya usajili wa makundi ya wachezaji (dancers) ambao wanapenda kucheza, kisha baada ya hapo hufanya mchujo katika vituo hivyo na kuchukua makundi matano ya washindi toka katika kila kituo na kuwapambanisha pamoja.

Lengo kuu la shindano hili ni kuwakutanisha vijana mbalimbali wenye uwezo wa kucheza ,na kisha kuwafanya wajulikane na watu tofauti kupitia kipindi hiki.

Washindi wanaopatikana katika shindano hili huzawadiwa fedha taslimu na zawadi nyinginezo kama zipo, kwa kuwapa zawadi washindi hawa huwafanya waweze kununua vifaa mbalimbali wanavyoviitaji katika sanaa yao na pia kuweza kufanya mambo yao mengine tofauti.

Washiriki katika shindano hili hucheza nyimbo mbalimbali zikiwemo reggae, R&B, Hip Hop na nyinginezo, na pia ili mtu aweze kushiriki anapaswa awe na kikundi cha wenzake kuanzia watu 5 hadi 8, mwenye afya njema, umri wa kuanzia miaka 18 (kama ana chini ya miaka hiyo anapaswa aje ana kibali toka kwa wazazi)