Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

TRA yakusanya Trilioni 3.84, maombi 1950 yatajwa

Monday , 8th Oct , 2018

Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA), imekusanya kiasi cha jumla ya shilingi trilioni 3.84 kwa mwaka wa fedha 2018/2019 sawa na ukuaji wa asilimia 5.32% ndani ya miezi 3, ikilinganishwa na shilingi trilioni 3.65 zilizokusanywa kipindi cha miezi hiyo kwa mwaka wa fedha 2017/2018.

Katika taarifa yake aliyoitoa leo mbele ya waandishi wa habari, Mkurugenzi wa Elimu na huduma kwa mlipa kodi TRA, Bw. Richard Kayombo amesema fedha hizo zilizokusanywa zimetokana na ongezeko la walipakodi nchini, ndani ya kipindi cha mwezi Julai, Agosti na Septemba mwaka huu.

"Katika mwezi Julai tulikusanya trilioni 1.2 sawa na 9.2%, Agosti tulikusanya trilioni 1.27 sawa na 5.86% na Septemba tulikusanya trilioni 1.36 sawa na 1.65%, kodi zote hizi zimetokana na kuongezeka kwa walipa kodi, kulipa kodi kwa hiari kote nchini, kwani kama TRA tumekuwa tukiendelea na juhudi za kuhakikisha elimu ya ulipaji kodi inawafikia wananchi." amesema Kayombo.

Aidha akitoa takwimu juu ya zoezi la kutoa msamaha wa riba na adhabu kwa wale wanaostahili kwa malimbikizo ya kodi za nyuma Bw. Kayombo amesema, "mpaka sasa tumepokea maombi 1950 kwa walipa kodi kote nchini yanayojumuisha riba na adhabu ya shilingi bilioni 185.4, ambapo maombi mengi yamejibiwa huku tukiendelea kuyafanyia uvumbuzi yale ambayo yamebaki na tunawaomba walipa kodi wajitokeze kwani mwisho wa zoezi hili ni Novemba 30, mwaka huu".

Pia Kayombo amewaonya wale wote wanaofanya udanganyifu katika risiti za 'EFD' kuacha kugushi na kutoa risiti zisizo halali, huku akisema tabia hiyo imesheheni maeneo ya biashara mitaa ya Kariakoo, jijini Dar es salaam na kuahidi kuwafikisha mahakamani wale wote watakaobainika na uvunjaji wa sheria hiyo.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu