Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Apandishwa cheo baada ya shitukizo la Magufuli

Tuesday , 15th May , 2018

Rais Dkt. John Magufuli amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James kumpandisha cheo Kaimu Kamishna wa Forodha na Ushuru wa Bidhaa wa TRA bandari ya Dar es Salaam Usaje Asubisye na kuwa Kamishna kamili bandarini hapo ndani ya wiki hii.

Dkt. Magufuli ametoa agizo hilo wakati alipokuwa anazungumza viongozi mbalimbali kwenye bandari ya Dar es Salaam mara baada ya kumaliza ziara yake ya kushtukiza kwenye bandari na kusema amefanya hivyo kutokana na kazi nzuri aliyoifanya Ben Usaje katika kusimamia maslahi ya nchi vizuri.

"Nawapongeza watu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kazi nzuri mnayoifanya,  Waziri wa Fedha kampeni tu huyu ukamishna kamili kwa sababu amesimamia haki halisi kwaajili ya maslahi mapana ya nchi yetu, najua wanamchukia sana wengine wafanyabiashara lakini waache wakuchukie Mungu anakupenda na watanzania tutaendelea kukupenda kwa hiyo mka-confirm. Katibu Mkuu mkazungumze wote mumpe angalau ndani ya wiki hii msimcheleweshe", amesema Dkt. Magufuli.

Uamuzi huo wa Rais Magufuli umekuja baada ya kumuuliza swali Kaimu Kamishna kuwa anafanya kazi gani TRA na ndipo alipotoa amri hiyo ya kupandishwa cheo haraka kutokana na kuwa ameweza kusimamia haki na maslahi kwa ufasaha.

 

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine