
Waziri wa ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi Profesa Anna Tibaijuka. Wizara yake ina ndiyo inayoshughulikia suala la fidia kwa wakazi wa Chasimba.
Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Basihaya Bw. Daniel Aron amesema kuwa mgogoro huo umetimiza miaka miwili sasa tangu serikali iahidi kushughulikia tatizo hilo, na kwamba kwa muda wote huo hawajaonyeshwa eneo watakalohamishiwa licha ya kuambiwa eneo hilo lipo tayari.
Bw.Aron amesema serikali iliahidi kuwapa maeneo au fidia ambapo mpaka sasa wakazi 3,060 wameshafungua akaunti katika benki mbalimbali ili kuwekewa fedha za fidia pasipo mafanikio.