Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kigaila amchonganisha IGP na Lugola

Thursday , 14th Feb , 2019

Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa CHADEMA, Bensoni Kigaila amehoji kati ya Waziri wa Mambo ya Ndani Kangi Lugola na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Simon Sirro nani atakuwa mkweli kuhusiana na uchunguzi wa shambulio la Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu.

Kushoto, IGP Sirro, Katikati ni Benson Kigaila na mwisho ni Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola

Bw. Kigaila amehoji hayo leo mchana Februari 14, wakati akizungumza na vyombo vya habari kutokana na kauli ya Waziri Kangi kusema kwamba shambulio la Lissu haliwezi kufanyiwa uchunguzi kutokana na kwamba kiongozi huyo kuwa mbali na nchi.

Kigaila amekumbusha kwamba kauli ya Waziri Lugola inakinzana na ile ya IGP Sirro ambaye mara  baada ya tukio la Lissu alisikika akisema kwamba tayari amekwishatuma makachero wake jijini Nairobi kumhoji Lissu.

"Leo Lugola anasema kwamba hawezi kutuma makachero wake nje. Sasa kwahiyo IGP alikuwa anadanganya? na kama alikuwa akidanganya alikuwa anadanganya kwa maslahi ya nani? ni kwanini shambulio la Lissu limekuwa na uwongo mwingi?", amehoji Kigaila.

Mbali na ushahidi wa Lissu, Kigaila amehoji ni kwanini mpaka sasa serikali haijawahoji mfanyakazi wa Naibu Spika, Askari waliokuwa lindoni siku Lissu anapigwa risasi  au kufanya uchunguzi  wa aina ya risasi na kisha kuja kuchukua ushahidi wa mwisho kwa waathirika ambapo ni Lissu na dereva wake.

Kuhusu ziara ya Lissu huko nchi za nje,Kigaila amesema kwamba chama chake kimebariki Mbunge huyo kwa asilimia zote katika ziara zake za nchini Marekani na huko Ulaya kwa kuwa dunia inapaswa kujua jambo Lissu alilotendewa.

HABARI ZAIDI

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari

Picha ya Diddy na Cassie enzi za mahusiano yake

Diddy aomba msamaha kumshambulia EX wake Cassie

Rais wa Iran Ebrahim Raisi

Rais wa Iran afariki kwa ajali ya Helikopta

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu