Monday , 20th Apr , 2015

Waziri Mkuu wa Zamani Edward Lowassa ameitaka Jumuiya ya Albino nchini Tanzania kuisukuma serikali ili rais Jakaya Kikwete asaini utekelezaji wa hukumu ya kuwanyonga wauaji wa albino.

Waziri Mkuu wa Zamani Edward Lowassa.

Mh. Lowassa ameyasema hayo wakati akihutubia mamia ya vijana walioshiriki matembezi ya hiari kulaani na kupinga mauaji, ukataji wa viuongo pamoja na ufukuaji wa makaburi ya albino Jijini Dar es Salaam.

Kauli hiyo ya Lowassa imekuja wiki moja tu baada ya Rais Kikwete kusema hajapelekewa majina ya watu 16 waliohukumiwa kifo kutoakana na mlolongo mrefu wa kisheria uliopo kabla ya kumfikia.

Aidha kutokana na kukithiri kwa mauaji hayo Lowassa ameiomba Serikali kuunda kamati maalumu itakayokuwa ikichunguza mauaji ya walemavu hao bila kutegemea kamati za mikoa ili kuongeza ufanisis wa kuilinda jamii hiyo.