Saturday , 29th Dec , 2018

Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) Seif Sharif Hamad, ameweka wazi mipango ya Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Freeman Mbowe baada ya kutoka gerezani ni kuungana na vyama vingine vya upinzani.

Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe

Katibu Mkuu huyo ameyasema baada ya kutumia siku ya Jumamosi ya leo kuwatembelea viongozi Mwenyekiti Mbowe pamoja na Mbunge Esther Matiko katika gereza la Segerea baada ya kufutiwa dhamana.

Maalim Seif amesema kwamba "Nimeitumia fursa ya kuonana na Mhe. Freeman Mbowe na Mhe. Esther Matiko kuwaeleza kuhusu  Azimio la Zanzibar na mikakati ya vyama sita vya siasa kurudisha demokrasia Tanzania. Mhe. Mbowe amenambia yuko pamoja na sisi na akitoka tu gerezani ataungana nasi kuendeleza atakapopakutia"

Aidha kiongozi huyo amebainisha kwamba viongozi hao wawili bado wapo imara na wana imani kwamba haki itatendeka juu yao.