
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe
Katibu Mkuu huyo ameyasema baada ya kutumia siku ya Jumamosi ya leo kuwatembelea viongozi Mwenyekiti Mbowe pamoja na Mbunge Esther Matiko katika gereza la Segerea baada ya kufutiwa dhamana.
Maalim Seif amesema kwamba "Nimeitumia fursa ya kuonana na Mhe. Freeman Mbowe na Mhe. Esther Matiko kuwaeleza kuhusu Azimio la Zanzibar na mikakati ya vyama sita vya siasa kurudisha demokrasia Tanzania. Mhe. Mbowe amenambia yuko pamoja na sisi na akitoka tu gerezani ataungana nasi kuendeleza atakapopakutia"
Aidha kiongozi huyo amebainisha kwamba viongozi hao wawili bado wapo imara na wana imani kwamba haki itatendeka juu yao.