Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mchungaji Lwakatare awatoa gerezani wafungwa 50

Thursday , 8th Sep , 2016

Zaidi ya wafungwa 50 waliokuwa wamehukumiwa kwenda jela kwa kushindwa kulipia faini za kiwango tofauti tofauti wameachiwa huru baada ya kupata msaada wa kulipiwa faini zao.

Mchungaji Getrude Lwakatare

Msaada huo umetolewa na aliyekuwa Mbunge wa viti maalum CCM Dkt. Getrude Lwakatare kwa gharama ya shilingi Millioni 25 ambapo kwa awamu ya kwanza ametoa wafungwa 50 na awamu ya pili itawahusu wafungwa 28.

Akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kutoa msaada huo katika magereza ya Ukonga, Keko na Segerea Dkt. Lwakatare amesema lengo kuu la kutoa msada huo ni kuisadia serikali kupunguza msongamano wa wafungwa magerezani.

“Hatutetei uhalifu, msaada huu siyo tu kupunguza wafungwa gerezani bali kurejesha nguvu kazi ya taifa na ndani ya familia kwani wazazi waliofungwa hapa ni masikitiko kwa familia na watoto wao, hivyo tumesaidia familia nyingi kurejesha amani na faraja kwao”

Aidha Dkt. Lwakatare amewaasa wale wote waliochiwa huru kutoka magerezani kuwa wananchi wema wanapoishi na kuacha kufanya vitendo vya uvunjifu wa amani na kujikita katika ujenzi wa taifa.

“Biblia inasema katika Mathayo 25:36 – 40 inasema kuhusiana na kuwaona walioko kifungoni, na mimi kama mtumishi wa Mungu nimeguswa kutimiza andiko hilo” amesema

Lwakatare amewataka wanaoguswa na tukio hilo kujitokeza kwa wakati mwingine kuwasaidia wale waliofungwa kwa kukosa fedha za faini ili warudi tena uraiani na kushiriki katika shuguli za uzalishaji mali na maendeleo

HABARI ZAIDI

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90