Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mgombea ACT,Njombe avamiwa wakati akifanya kampeni

Thursday , 15th Oct , 2015

Mgombea wa ACT-Wazalendo jimbo la Njombe Kusini, Emilian Msigwa amenusurika kupigwa na watu wanao daiwa ni wafuasi wa chama cha mapinduzi (CCM) akiwa katika mkutano wa kampeni za uchaguzi.

Mgombea wa ACT-Wazalendo jimbo la Njombe Kusini, Emilian Msigwa akiongea na Wanakijiji cha Ihanga

Akizungumza na waandishi wa habari mkoani Njombe Mgombea huyo amelalamika kuhusiana na vurugu hizo leo akisema kuwa zilitokea juzi katika mkutano wake uliokuwa ukifanyika katika kijiji cha Yakobi cha jimbo hilo.

Msigwa amesema kuwa katika kata ya Yakobi amekuwa akipata shida ya kufanya kampeni katika vijiji vyake kutokana mgombea udiwani wa kata hiyo kupitia CCM kuweka vikwazo vya kuzuia mikutano ya chama hicho kwa kuweka ratiba zake na kufanya hujuma na watendaji wa vijiji hivyo.

Akizungumzia ulinzi wa polisi katika mikutano yao alisema kuwa katika mikutano yao mingi ya vijiji huwa wanaenda bila ya kuwa na polisi kutokana na umbali wa maeneo na kuwa na imani ya kuwa na amani katika maeneo hayo na kusema kuwa mikutano ya mjini huwa wanakuwa na polisi.

Msigwa ameongeza kuwa ameshiriki chaguzi nyingi lakini hajawahi kuona CCM wanafanya vurugu kama vyama vingine lakini mwaka huu ni tofauti na kuwa CCM wamebanwa.

Akizungumza na kituo hiki kwa njia ya simu kamanda wa polisi mkoa wa Njombe, Wallboard Mtafungwa, amesema kuwa tukio hilo limewafikia na kuwa wanamshikilia Erasto Ngole (43), mkazi wa Itulike mkoani humo mwanachama wa CCM na wengine saba wanatafutwa kuhusiana na tukio hilo.

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine