Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mwili wa Mama Mercy Anna Mengi waagwa

Thursday , 8th Nov , 2018

Askofu wa Kanisa la Kiinjili Kiluteri Tanzania (KKKT), Dayosisi na Mashariki na Pwani, Askofu Alex Malasusa amewataka watu waendelee kumuombea aliyekuwa moja ya waanzilishi wa makampuni ya IPP Mama Mercy Anna Mengi ambaye alifariki dunia Oktoba 31 mwaka huu.

Familia ya Mama Mercy Anna Mengi wakiwa kanisani Azania Front katika ibada ya kuaga mwili wa marehemu.

Akizungumza katika ibada maalum ya kuuaga mwili wa marehemu Mama Mercy Anna Mengi ambao ilihudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa kitaifa ambapo Askofu Malasusa alinukuu neno la Biblia kutoka Paulo 4 mstari 13 hadi14 na Paulo 5 mstari 1 hadi 2.

Jambo kubwa na la maana kwetu sisi ni kuwa na uhakika kwa mungu kwa kushika na mapenzi yake, na hata katika hili tuyakubali mapenzi yake kama inavyosema sala yake, ili tuendelee kuishi kwa mapenzi yake,” amesema Dkt Alex Malasusa.

Askofu Malasusa amesema “Mungu ameweka siri kubwa kwenye suala la kifo, hata sisi wachungaji Mungu ametuficha bali ni siri yake yeye mwenyewe Mungu, niwaombe ndugu jamaa tuendelee kujiweka karibu nayeye ili kila mtu afikie tamanio la kwenda mbinguni.”

Miongoni mwa watu walioshiriki ibada hiyo ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli, Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda.

Ibada hiyo iliyofanyika Jijini Dar es salaam, ilianza majira ya saa 6 mchana na kuongozwa na Askofu wa kanisa hilo,  Dkt Alex Malasusa akisaidiwa na msaidizi wake Chadiel Luiza.

Mwili wa Mama Mercy Mengi unatarajiwa kusafirishwa kuelekea Machame Moshi kwaajili ya maziko Jumamosi Novemba 10, 2018.

Mama Mercy Anna Mengi atakumbukwa kama moja ya waanzilishi wa makampuni ya IPP ambayo inamiliki vyombo mbalimbali vya habari ikiwemo EATV, EA Radio, ITV, NIPASHE, The Guardian, Radio One, na Capital Radio.

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine