Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Rais Magufuli apangua safu za wakurugenzi

Monday , 13th Aug , 2018

Rais Dkt. John Magufuli amefanya mabadiliko madogo ya wakuu wa wilaya pamoja na kuteua wakurugenzi wapya 41 wa halmashauri za wilaya, miji na manispaa huku akiwahamisha vituo wakurugenzi 19, kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za kujaza nafasi zilizowazi.

Rais Dkt. John Magufuli

Katika mabadiliko hayo, Rais Magufuli pia amembadilisha kituo cha kazi mkuu wa wilaya ya Kwimba, Mhandisi Msafiri Simeoni na kuwa Mkuu wa Wilaya ya Chato na kumteua Senyi Simon kuenda kushika nafasi yake.

Akisoma uteuzi huo Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi amewataka wakurugenzi wote wapya kuripoti siku ya Jumatano, Agosti 15, 2018 katika ofisi za Katibu Mkuu wa TAMISEMI pia watakapokwenda Dodoma wanapaswa kuwa na vyeti vyao vya kidato cha nne, sita na elimu ya taaluma.

"Wakurugenzi ambao katika mabadiliko haya wamebadilishwa vituo vya kazi, wanapaswa kwenda kuripoti katika vituo vyao vya kazi mara moja. Na kwa wale wakurugenzi walioteuliwa kwa mara ya kwanza wanatakiwa kuripoti kwa Katibu Mkuu wa TAMISEMI Agosti 15 mwaka huu kwa ajili ya kiapo cha uadilifu na maelekezo ya majukumu yao", amesema Balozi Kijazi.

Mbali na hilo, Rais Magufuli amemuamisha kituo cha kazi aliyekuwa Mkurugenzi wa Kakonko Mkoa wa Kigoma Lusubilo Mwakabili na kuwa mkurugenzi wa halmashauri ya Temeke. Pia amemteua Beatrice Kwai kuwa mkurugenzi wa halmashauri ya Ubungo na Mwilabu Nyabusu amemteua kuwa mkurugenzi wa halmashauri ya Kigamboni.

Uteuzi huo wa Rais Magufuli unakuwa wa pili kufanyika kwa kufanya mabadiliko makubwa katika safu ya uongozi ambapo wa kwanza ulikuwa ni Julai 28, 2018 ambapo aliteua wakuu wa mikoa, wilaya pamoja na makatibu tawala.
.

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine