Friday , 9th Dec , 2016

Mkuu wa Mkoa wa Ruwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen Zelote amewaagiza wakuu wake wa wilaya kwa kushirikiana na halmashauri zao pamoja na wananchi kuwa na kiwanda angalau kimoja ili kutekeleza kauli mbiu ya maadhimisho miaka 55 Uhuru kwa vitendo

Mkuu wa mkoa wa Rukwa - Zelothe Stephen

Ameyasema hayo wakati alipomaliza kupanda mti kama ishara ya maadhimisho ya siku ya uhuru yaliyofanyika katika viwanja vya ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa kushirikiana na watumishi wote wa ofisi yake.

Amewataka watumishi wote kila mmoja kuwa na mti wake ambao atauhudumia hadi kukua kwa mti huo, hii ikiwa ni mwanzo wa kampeni ya upandaji miti ili kuokoa Mkoa wa Rukwa kugeuka kuwa jangwa.

Katika kutekeleza Kauli mbiu ya siku ya Uhuru wa Vitendo Mkuu wa Mkoa amezitahadharisha halmashauri hasa idara ya ardhi, elimu, afya na mahakama juu ya kukithiri kwa rushwa.