Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Sakata la waandishi,CHADEMA yanena Uhamiaji yajibu

Thursday , 8th Nov , 2018

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimejitokeza juu ya kushikiliwa kwa waandishi wa habari wawili ambao ni Raia wa kigeni na wanaharakati wa kamati maalum ya kuwalinda wanahabari Duniani CPJ.

Mkurugenzi wa Itifaki na mambo ya nje wa CHADEMA, John Mrema, Mrakibu wa Polisi, Msemaji Idara ya Uhamiaji, Ally Mtanda.

Waandishi hao waliokamatwa ni Mkuu wa kamati ya Afrika, Angela Quintalna Muthoki Mumo ambaye ni mwakilishi wa kamati hiyo ya Afrika mashariki.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam Mkurugenzi wa Itifaki na mambo ya nje wa CHADEMA, John Mrema ameitaka idara ya uhamiaji nchini kurejesha Passport zao ili kuwapa nafasi waandishi hao wa kigeni kufanya kazi kwa uhuru.

"tunaitaka idara ya uamiaji ituambie imetumia sheria gani kuwakamata waandishi hao wa kigeni, pia tunaitaka serikali iseme kwa uwazi nani alitoa amri ya kukamatwa kwa waandishi hawa, na mwisho iboreshe maisha ya kufanyia kazi kwa waandishi wa habari."

Mapema jana ilielezwa kuwa Maafisa waliojitambulisha kuwa wanatoka Idara ya Uhamiaji, waliwakamata viongozi wao katika Hoteli waliyofikia jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo Jijini Dar es salaam, Mrakibu wa Polisi, Msemaji Idara ya Uhamiaji, Ally Mtanda amesema waliwashikilia waandishi hao wawili na leo hii wamerejeshewa pasipoti zao.

"Ni kweli tuliwashikilia kwa muda, tulifanya mahojiano nao, tulizikamata paspoti zao na sasa tumewarejeshea. Tumewaelekeza wafuate taratibu lakini tumewakabidhi pasipoti mbele ya ubalozi wao," amesema Ally Mtanda.
 

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine