Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Shule za binafsi zapigwa marufuku kupandisha Ada

Thursday , 10th Jan , 2019

Naibu Waziri wa TAMISEMI, Mwita Waitara amepiga marufuku kupandishwa kiholela kwa ada na michango isiyo na tija kwa shule za Umma na binafsi jambo ambalo limekuwa kero siku za hivi karibuni.

Naibu Waziri wa TAMISEMI, Mwita Waitara

Akiongea leo, Januari 10 jijini Dar es salaam, Waitara amesema kumekuwepo na malalamiko mengi kipindi hiki cha shule kufunguliwa kuwa shule za binafsi zimekuwa zikitoa maelekezo ya ada kupanda bila kukubaliana na wazazi.

''TAMISEMI tumeshatoa utaratibu kwa shule zote lazima kila jambo liwe shirikishi kwa wazazi, kama ni ada au mchango lazima kuwepo na majadiliano na makubaliano ya kikao bila hivyo ni kuvunja utaratibu'', amesema.

Waitara amesisitiza kuwa hatua kali zitachukuliwa kwa wale wote wanaokiuka maelekezo ya serikali ikiwemo kutowahusisha wazazi katika kupandisha ada jambo ambalo linatakiwa lifanyike kabla ya shule kufungwa na sio ghafla tu wakati wa shule kufunguliwa.

Mbali na hilo Waitara ametoa siku 90 (miezi mitatu), kwa wazazi kuweza kupeleka watoto wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza kwenye shule za serikali na endapo hawatafanya hivyo nafasi hizo zitabaki wazi au zitachukuliwa na wengine.
 

HABARI ZAIDI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali