Kauli hiyo imetolewa Jijini Dar es Salaam na wajumbe wa Kamati hiyo wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati Bi. Margaret Munyagi wakati walipotembelea vituo vya East Africa Television (EATV), East Africa Radio, ITV/ Radio One pamoja na Capital Television na Capital Radio.
Pamoja na mambo mengine wajumbe wa Kamati ya Maudhui ya TCRA wamevipongeza vituo vya IPP kwa kwenda na wakati kutokana na kutumia vifaa vya teknolojia ya kisasa katika utangazaji ambavyo vimekuwa vikiboresha ubora na kuongeza ufanisi wa kazi.