
Akiongea na East Africa Radio Mwenyekiti wa Soko hilo Bw Saidi Habibu amesema kuwa hapo awali kulikuwa hamna takwimu sahihi za wafanyabiashara hao hali iliyopelekea ugumu katika kukusanya mapato na upatikanaji wa huduma nyingine za kijamii kama upanuzi wa soko.
Aidha, Bw Habibu amesema kuwa soko hilo linakabiliwa na ufinyu wa miundombinu hivyo halina uwezo wa kupokea wafanyabiashara wapya watakaoondolewa katika maeneo yasiyo rasmi.