
Fatma Karume kushoto na Hamis Kigwangalla kulia.
Viongozi hao wawili wanakutana katika mzungumzo ambayo yanahusisha chakula cha katikati ya asubuhi na mchana maarufu kama 'Brunch' ambayo wao wameamua kuiita 'Brunch date' huku kila mmoja akitamba ataibuka mshindi kwa kula pamoja na hoja.
Mapema leo Fatma ameanzia kwenye mazoezi huku akimtahadharisha Kigwangalla kuwa mazoezi hayo ni kwaajili yake hivyo ajipange na 'Wallet' yake vinginevyo atakosa pesa ya kulipia na ataosha vyombo'
Wallahi @HKigwangalla I am not going DUTCH for this BRUNCH. I mean it so you really had better come with your WALLET. Maana nitakuacha pale Hyatt usafishe vyombo mimi nitasepa !
— fatma karume aka Shangazi (@fatma_karume) January 13, 2019
Naye Kigwangalla amejibu kwa kumtishia Shangazi kuwa atamshinda na endapo atamletea uzungu mwingi kwasababu ni mtoto wa kishua na yeye ni mtoto wa uswahilini atatumia lugha ya Kinyamwezi kummaliza.
Ndiyo nimetoka mazoezini sasa hivi, nimearifiwa shangazi anajipanga! Haya bhana, tutaona leo nani Konki zaidi!
— Dr. Kigwangalla, H. (@HKigwangalla) January 13, 2019
'Brunch date' yao hiyo ilianza kwa mabishano ya hoja katika mtandao wa Twitter kabla ya kukubaliana wakutane kushindanisha hoja hizo katika hoteli ya Hyatt jijini Dar es salaam ndipo Shangazi akamwambia ahakikishe na msosi wa kutosha unakuwepo.
Wawili hao wakiwa njiani kuelekea eneo la tukio.
Njiani tayari kwa mnuso @HKigwangalla pic.twitter.com/ZLqA2iBJ89
— fatma karume aka Shangazi (@fatma_karume) January 13, 2019
Njiani tayari kwa mnuso! pic.twitter.com/vJBFPGPtI2
— Dr. Kigwangalla, H. (@HKigwangalla) January 13, 2019