Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wananchi wakimbia hospitali kisa waganga wa jadi

Friday , 15th Feb , 2019

Changamoto ya upatikanaji wa huduma za Afya katika kijiji cha Nyang’holongo Kata ya Nundu Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale Mkoani Geita imekuwa kubwa, hali inayopelekea wananchi kukimbilia kwa waganga wa jadi kupata huduma hizo.

Baadhi ya vifaa vya waganga wa jadi

Imeelezwa kuwa sababu za baadhi ya wananchi kufuata huduma za matibabu kwa waganga wa jadi ni huduma za afya kuwa umbali mrefu kwani wanalazimika kutembea umbali wa kilomita 10 kwenda katika Zahanati ya kata jirani ya Bukwimba ama wanasafiri kwenda makao makuu ya Wilaya kwenye kituo cha afya Kharumwa takribani kilomita 25.

Marko Mwiyabule ni Mwenyekiti mwanzilishi wa kijiji hicho tangu mwaka 1974 na kustaafu mwaka 2004, ambapo  anasema wananchi wamekuwa wana mwamko hali iliyopelekea kuchangia  Sh. elfu sitini kwa lengo la kujenga zahanati ambapo afisa Mtendaji wa Nyang’holongo Masumbuko Robert amesema walifikisha milioni 22 ambazo walinyanyua boma.

Kutokana na changamoto hizo zinazowakabili wananchi, Mgodi wa Dhahabu wa Acacia Bulyanhulu kutoka Mkoani Shinyanga umeguswa na kutoa msaada wa vifaa vya ujenzi vyenye thamani ya zaidi ya Milioni 67.

Akipokea vifaa hivyo Mkuu wa wilaya ya Nyang’hwale, Hamimu Gwiyama amesema kiongozi kutoka ngazi ya wilaya kwa mara ya mwisho alifika kijijini hapo mwaka 2005 yapata miaka 14 sasa.

Aidha uongozi wa kijiji umesema kuna wakazi wapatao 2598 na kwamba waliochangia fedha kama nguvu za wananchi ni wakazi 502 hivyo wamejielekeza kuleta msukumo zaidi ya ili watu wote washiriki kikamilifu kwenye miradi ya maendeleo.
 

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine