Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Warioba afichua siri nzito siku ya uhuru

Saturday , 8th Dec , 2018

Waziri Mkuu wa 5 wa Tanzania, Joseph Warioba amefunguka juu ya tarehe 9 Disemba, siku ya ambayo Tanzania imekuwa ikisheherekea kupatikana kwa uhuru, ambapo ameeleza kwa wakati huo kuendesha nchi ilikuwa ni kitu kigumu sana kwa sababu kulikuwa na wasomi wachache.

Waziri Mkuu wa 5 wa Tanzania, Joseph Warioba.

Kwa mujibu wa Warioba ambaye kwa sasa ana miaka 78, wakati Tanganyika inapata uhuru yeye alikuwa na miaka 21 na kwa wakati huo nchi nzima ilikuwa na wahandisi wawili tu.

"Nakumbuka nilikuwa kijana wakati ule, na tulikuwa kwenye mapambano ya kupata uhuru, na tulishangazwa sana kuona bendera ya mkoloni inashushwa na bendera yetu ya Tanganyika inapanda, na baada ya hapo Mwalimu Nyerere alitushinikiza tufanye kazi kwa bidii." Amesema.

"Wakati tunapata uhuru kulikuwa na ubaguzi, waafrika tulikuwa tunaonekana ni watu wa hali ya chini, lakini siku hiyo tukaanza kujiona ni binadamu kama binadamu wengine." Ameongeza Warioba.

"Ni kweli wakati ule kulikuwa na wasomi wachache sana, mfano wahandisi nchi nzima walikuwa wawili tu na ukija kwenye taaluma nyingine walikuwa ni wachache tu japo mipango ilishaanza kuwepo ya kuwa na wasomi, ndiyo maana miezi miwili kabla ya uhuru kikafunguliwa chuo kikuu." Amesema.

Ameongeza kuwa kuhusu usafiri kipindi kile hali ilikuwa ngumu sana, ukilinganisha na sasa hivi, ambapo tumeendelea sana, kila kona kuna lami maeneo na yanafikika kwa urahisi.

Disemba 9, Tanzania inaadhimisha miaka 57 ya uhuru, ambapo Rais Magufuli licha ya kuwasihi watanzania kuendelea kufanya kazi pia aliamuru kiasi cha fedha kilichopangwa kutumika kwenye maadhimisho hayo kikatumike kujenga hospitali ya Uhuru Jijini Dodoma pamoja na kutangaza kuwasamehe wafungwa 1,076.

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine