Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu vijana, Ahmad Alhendawi
Kwa siku tatu vijana kutoka pande mbali mbali za dunia wanakutana jijini Nairobi, kwenye jukwaa la kwanza kabisa la vijana kwenda sambamba na mkutano wa kamati ya biashara na maendeleo ya Umoja wa Mataifa, UNCTAD.
Ahmad Alhendawi, baada ya kuzungumza nao, ukosefu wa ajira ukiwa tatizo kubwa, amesema, kila mtu anarushia lawama mwenzake; waajiri wanadai vijana hanawa stadi, vijana wanasema hawapati mitaji, sekta binafsi inadai sera si rafiki..vijana wakisalia kuwekwa rehani kutokana na ukosefu wa uratibu wa mipango.
Mjumbe huyo amesema kuwa inapaswa kuwaleta hawa wadau pamoja na vyuo vya elimu, sekta binafsi na wadau wa biashara pamoja na serikali na wadau wa maendeleo ili wazungumze pamoja ili hatimaye sera wanazobuni ziwekeze zaidi kwa vijana.