Wednesday , 1st Feb , 2017

Rapa Joh Makini ambaye hivi sasa anafanya vyema na ngoma yake 'Waya' amefunguka na kusema kuwa wao kama Weusi hawashindani na msanii yoyote yule ila wao wanafanya muziki katika kutimiza ndoto zao.

Joh Makini

 

Joh Makini alisema hayo kwenye kipindi cha Friday Night Live cha EATV na kusema wao kama Weusi wanafanya muziki ili kutangaza nchi, kutimiza ndoto zao katika maisha na si kushindana na msanii yoyote yule.

"Watu kwanza wanatakiwa wajue sisi hatushindani na mtu yeyote kwenye muziki huu watu wasichanganye vitu, sisi tupo hapa kwa ajili ya kutengeneza ndoto zetu, kuendesha maisha yetu na kuitangaza nchi yetu Tanzania kupitia hiki ambacho ametubariki" alisema Joh Makini 

Mbali na hilo Joh Makini aliizungumzia ngoma mpya ya Fid Q 'Kemosabe' na kusema ni ngoma kali sana na yeye amependa jinsi ambavyo Fid Q amebadilika katika flow kwani imekuwa tofauti na kazi zake nyingi za nyuma.

Fid Q

"Ngoma kali sana nimependa jinsi ambavyo Fid Q amebadilika katika flow kwani kazi hiyo imekuwa tofauti na kazi zake nyingi alizofanya kipindi cha nyuma' alisema Joh Makini