Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Usahili wa mwisho Dance 100% wakamilika kwa mtiti

Saturday , 8th Aug , 2015

Usahili wa mwisho wa Dance 100% 2015, umekamilishwa katika viwanja vya Leaders Club Kinondoni jij

Makundi matano yaliyoingia robo fainali leo yakiwa katika picha ya pamoja.

Usahili wa mwisho wa Dance 100% 2015, umekamilishwa katika viwanja vya Leaders Club Kinondoni jijini Dar es Salaam, muamko mkubwa wa makundi yapatayo 28 kutoka ndani na nnje ya mkoa yakiongezea ushindani na burudani zaidi katika michuano hiyo kuelekea kupata makundi mengine 5 yatakayoshinda uchaguzi.

Katika michuano ya leo, Wazawa Crew, The Best, Quality Boys, Majokeri na kundi la wasichana la Cute Babies waliweza kuwashawishi majaji na kuweza kujivunia alama nyingi zaidi zilizowawezesha kushinda nafasi ya kuingia robo Fainali ya Dance 100% 2015.

Wakizungumza baada ya kukamilika kwa usahili, Jaji wa Dance 100% 2015, Shetta amesema kuwa amefurahishwa kuona madansa wamejipanga zaidi, akitarajia mchuano mkali hatua inayofuata kutokana na makundi yote yaliyopita kuwa na uwezo mkubwa, wakati Jaji Queen Darleen akitoa wito kwa Madansa kuwa wepesi kuwahi nafasi za Usahili wakati mwingine kutokana na ushindani mkali wa leo kusababisha makundi mengine kupoteza nafasi kwa kukosa alama chache sana.

Jaji Super Nyamwela ambaye pia ni Dansa mkongwe, ameleeleza kufurahishwa kwake na namna makundi yalivyoonyesha kujipanga leo, na kuwapatia nafasi ya kuchagua vipaji bora zaidi, akifananisha usahili huo kama fainali ya mashindano kutokana na mchuano mkali ulioonyeshwa.

"Usahili huu uliofanyika hapa Leaders Club, umekuwa ni mkubwa zaidi, na kwa kuthibitisha ukubwa wa mashindano haya, kumekuwa na makundi yaliyosafiri kutoka mikoani Arusha na Mbeya kuja kushindana, japokuwa ushindani ulikuwa mkali sana na hawakuweza kupita, dalili inayoashiria hatua inayofuata itakuwa ni yenye msisimko zaidi", Alisema Happy Shame, Mratibu wa michuano hiyo kutoka EATV.

Makundi mwengine ambayo yameshiriki katika usahili leo ni Best Plan, A Town Dancers kutoka Arusha, Boko Young Talent, The Quest Crew, TNT, Tatanisha, DMX, House of Kinetix, Majokery, Sababisha, The World Of Champions, Makaba Crew, Hamadombe, Mazabe Powder, Snap Boys Crew, Bustani Dancers, TGE Hardware, Best love, Chipukizi Dancers, Danger Boys, Butterfly kutoka Mbeya, Bata Boys na Fresh Crew.

Kujionea yote yaliyojiri leo, usisahau kutazama shoo ya Dance 100%, Jumamosi ijayo saa 12:30 jioni EATV pekee.

Dance 100% 2015 inaletwa kwako na EATV na East Africa Radio na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania na Coca Cola, Kinywaji rasmi cha Dance 100% kwa mwaka huu.

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine