Wednesday , 19th Mar , 2014

Msanii wa Muziki Z Anto, ambaye ametokea huko Kenya kwa ajili ya kufanya shoo iliyokosa wahudhuriaji, ameibuka na kulitolea ufafanuzi suala hili ambalo linaweka rekodi mbaya kabisa katika historia ya muziki wake.

Z Anto ameongea na eNewz kwa kirefu na kusema kuwa, katika ziara yake huko Kenya, alipata changamoto mbalimbali kutokana na muandaaji wa shoo aliyekuwa anafanya naye kazi kutokuwa mwaminifu, ambapo pia msanii huyu amekanusha taarifa za yeye kuishiwa kiasi cha kukosa nauli baada ya maonyesho yake kufeli.

Huyu hapa Z Anto akielezea zaidi suala zima la ziara yake hiyo
ilivyovurundwa.