
Nyota huyo amekamilisha vipimo vya afya jijini Barcelona usiku wa kuamkia leo na atasaini mkataba wa miaka mitano na nusu. Coutinho ameigharimu Barcelona kiasi cha £142m, takribani shilingi milioni 383.
Barcelona itaanza kulipa kiasi cha £ 105m na kiasi kingine kitakuwa kinalipwa kutokana na kiwango atakachoonesha nyota huyo mwenye umri wa miaka 25. Coutinho alisajiliwa na Liverpool Januari 2013 kutoka Inter Milan kwa dau la £ 8.5m.
Coutinho sasa anakuwa mchezaji wa kwanza kutoka ligi kuu ya England kuuzwa kwa fedha nyingi rekodi ambayo ilikuwa inashikiliwa na Gareth Bale ambaye alinunuliwa kwa dau la £80m kutoka Tottenham kwenda Madrid.
Coutinho pia anakuwa mchezaji wa pili kusajiliwa kwa gharama kubwa akitanguliwa na Mbrazil mwenzake Neymar ambaye alisajiliwa na PSG kutoka Barcelona kwa dau la £222m.
Philippe Coutinho anaweza kuzidiwa na nyota wa PSG Kylian Mbappe ambaye amenunuliwa kwa mkopo kutoka Monaco lakini atanunuliwa kwa dau la £166m msimu ujao.