Mfumo huo utatumika endapo timu zitalingana kila kitu na lazima bingwa apatikane hivyo watautumia mfumo huo ukiwa na maana wataangalia matokeo ya timu hizo mbili walivyokutana kwenye michezo yao.
“Tumepata funzo kwenye michuano Afrika kwa vijana iliyomalizika hivi karibuni kule Gabon, kama mtakumbuka timu yetu iliondolewa kwa sheria hii baada ya kufungwa na Niger na kujikuta wakiwa na matokeo yaliyofanana…, na sisi tutaingiza mfumo huu kwenye ligi yetu, tutalijadili kwenye mkutano wa TFF,” alisema Malinzi.


