Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ni nani wa kumuamini taarifa zake TFF?

Tuesday , 4th Jun , 2019

Kuna mkanganyiko mkubwa unaendelea hivi sasa juu ya taarifa mbalimbali zinazotolewa na Shirikisho la Soka Tanzania TFF kwenye mashindano inayoyasimamia.

Sintofahamu ya TFF na Kapombe

Kwa mujibu wadau mbalimbali wa soka, inawatia wasiwasi mkubwa kuziamini taarifa za moja kwa moja kutoka kwa kiongozi yoyote wa shirikisho hilo kutokana na siku za hivi karibuni mmoja wa kiongozi wake kutoa taarifa kuwa Kagera Sugar imeporomoka ligi na baadaye kukanushwa na kiongozi mwingine, pia taarifa nyingine ni juu ya majeraha ya mlinzi wa Simba, Shomari Kapombe.

Suala la Kagera Sugar kushuka daraja, mara baada ya ligi kumalizika, Afisa Habari wa TFF, Cliford Ndimbo alikaririwa kuwa timu hiyo ndiyo itakayoungana na African Lyon kushuka daraja moja kwa moja, lakini baada ya muda mfupi, Mkurugenzi wa Bodi ya Ligi, Boniface Wambura alikanusha taarifa hiyo na kusema kwamba kuna kiongozi alifanya uzembe wa kuweka taarifa zisizo sahihi katika msimamo wa ligi. Aliirudisha Kagera Sugar katika Playoff na kuahidi kutoa adhabu stahiki kwa kiongozi aliyehusika katika upotoshaji huo.

Jana, Juni 3 pia kumekuwepo na mkanganyiko juu ya taarifa ya majeraha ya mlinzi wa Simba na timu ya taifa, Shomari Kapombe ambaye aliitwa katika kikosi cha Taifa Stars kinachokwenda nchini Misri. Afisa Habari wa TFF alikaririwa akisema kuwa Shomari amejitonesha majeraha katika mazoezi na timu ya taifa, ambapo hali yake inaangaliwa kama ataweza kuwa fiti kabla ya michuano.

Baada ya muda mfupi, Kapombe alikanusha taarifa hiyo akisema kuwa hajajiunga na kambi ya timu ya taifa na anaendelea na mazoezi yake binafsi kama alivyoagizwa kocha wake wa Simba, huku akiwataka watu kuacha kusambaza taarifa hizo za uongo.

Kutokana na mikasa hiyo, inaonesha kuwa kuna uwasilishaji mbovu wa taarifa kutoka TFF, jambo ambalo limepelekea kuwepo kwa mashaka kwenye ukweli wa kila taarifa ambayo itakuwa inatoka kwenye shirikisho kwenda kwa wadau wa soka nchini.

HABARI ZAIDI

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90