Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Simba na Yanga watambiana matawini

Tuesday , 21st Feb , 2017

Kuelekea katika mpambano wa watani wa jadi Simba na Yanga, viongozi wa matawi mbalimbali ya vilabu hivyo wameendelea kutambiana huku wakiitaka serikali kumchukulia hatua mtu yeyote atakayegundulika kufanya uharibifu katika mchezo huo.

Mashabiki wa Simba na Yanga Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam

Mwenyekiti wa tawi la Mpira Pesa kwa upande wa Simba Ostadh Masoud amesema, mechi zote wanazokutana na Yanga wanaziheshimu na kikosi cha Simba kimejipanga vizuri na kwa umakini ili kuweza kuibuka na ushindi kwani lengo lao hasa ni ubingwa ili kuweza kuiwakilisha nchi katika mashindano ya kimataifa.

"Lazima tuongeze umakini kwasababu Yanga tulimkimbia kwa pointi nane leo hii ametukuta tunatofautiana kati ya pointi moja au mbili kwa hiyo anaonekana kuna kitu anakitaka kwa maana hiyo lazima niwaambie wana Simba hata wachezaji kwa ujumla hii ni fainali na kila mtu ambaye anaamini ana kitu ambacho kitasaidia Simba ishinde kitumike, " amesema.

Kuhusu vurugu, Ostadh amesema "Mimi niwaambie tuu mashabiki kuwa watulivu katika mchezo wa Februari 25, Mwamuzi akishapuliza kipyenga hakuna wa kupinga hata ukienda mahakama kuu, sisi tujikite kuhakikisha timu yetu inashinda na tusitegee kushindwa au sare, " amesema.

Kwaupande wake Katibu wa tawi Yanga la Tandale kwa Mtogole Waziri Jitu amesema, wanaamini wataibuka na ushindi katika mchezo huo kwani kikosi chake ni bora na Simba wasitegemee kama wataweza kubeba pointi tatu katika mchezo huo.

"Sisi tunajiamini na kazi tumeshamaliza tusubiri tuu siku ya jumamosi tufike Uwanjani kuhitimisha, mimi nina timu bora kwani Afrika Mashariki hii ikiangalia timu bora ya kwanza Yanga na inafuatiwa na Azam FC kidogo, " amesema.

HABARI ZAIDI

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari

Picha ya Diddy na Cassie enzi za mahusiano yake

Diddy aomba msamaha kumshambulia EX wake Cassie

Rais wa Iran Ebrahim Raisi

Rais wa Iran afariki kwa ajali ya Helikopta

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu