Thursday , 23rd Mar , 2017

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limempongeza Mheshimiwa Dk. Harrison Mwakyembe kwa kuteuliwa kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Dkt. Harrison Mwakyembe

Katika taarifa iliyotolewa leo kwa wana habari, imesema kuwa shirikisho hilo linaamini chini ya uongozi wake mahiri Tanzania itapiga hatua kubwa zaidi katika maendeleo ya michezo.

Naye Rais wa TFF, Jamal Malinzi kupitia mtandao wa twitter amesema "TFF inampongenza Dkt. Harrison Mwakyembe kwa kuteuliwa kuwa Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo.Tunakuombea mafanikio makubwa.Amina."