Tuesday , 25th Dec , 2018

Mshambuliaji wa Tanzania Thomas Ulimwengu amesaini mkataba wa miaka miwili kuichezea klabu ya JS Saoura ya Algeria.

Thomas Ulimwengu akiwa na mabosi wa JS Saoura.

Ulimwengu amesaini mkataba huo leo ambapo klabu yake hiyo ipo miongoni mwa timu 16 zilizoingia hatua ya makundi ya klabu bingwa Afrika sambamba na Simba SC ya Tanzania.

Usajili huu wa Ulimwengu umekuja ikiwa ni miezi miwili tu imepita tangu avunje mkataba na klabu ya Al Hilal ya Sudan ambayo hata hivyo hakuweka wazi sababu za kuvunja mkataba na timu hiyo ndani ya miezi mitatu tu.

Klabu ya JS Saoura imethibitisha usajili huo kwa kuweka picha ya Ulimwengu akiwa na mabosi wa timu hiyo akikabidhiwa jezi tayari kwa kukipiga.

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

عااااجل إدارة شبيبة الساورة تظفر بخدمات مهاجم المنتخب التنزاني و اللاعب الثاني خلال هذه الإنتقالات الشتوية - الإسم : أوليموانقو اللقب : توماس إيمانويل المنصب : مهاجم الفريق السابق : الهلال السوداني-تيبي مازمبي المنتخب : تنزانيا تاريخ و مكان الميلاد : 14 جوان 1993 بدار السلام (تنزانيا) #jssaoura #شبيبة_الساورة #رابطة_أبطال_إفريقيا #جيبوها_يا_لولاد #أدغال_إفريقيا_تناديكم

A post shared by Jssoura-شبيبة الساورة (@jssaoura.officiel) on

Ulimwengu huenda akakutana na Simba kwenye hatua ya makundi ya klabu bingwa Afrika kama ilivyokuwa kwa Yanga kwenye hatua ya makundi ya kombe la shirikisho mwaka 2016 alipokuwa akichezea TP Mazembe.