Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

''Yanga na Azam FC wanapanga matokeo''- Manara

Thursday , 17th Jan , 2019

Katika kipindi cha miaka kadhaa ambayo Simba haikushiriki michuano ya kimataifa, msemaji wake Haji Manara alikuwa akipambana na Bodi ya ligi (TPLB) juu ya Yanga na Azam FC kuwa na viporo vingi na kufikia hatua ya kusema wanapanga matokeo.

Haji Manara

Hivi sasa mambo yamegeuka na huenda Haji Manara anatamani maneno haya, ''Kama ambavyo Yanga na Azam FC wanapanga matokeo'', yafutike lakini teknolojia imetunza na yanatumika kama kumbukumbu ikimkumbusha kuwa mambo yamegeukia kwake wakati huu ambao Simba ina viporo 7 vya ligi kuu soka Tanzania bara.

Akiwa kwenye moja ya mikutano ya klabu na wanahabari miaka iliyopita Manara alisema, ''Kwa kawaida timu inatakiwa kucheza mechi moja na kupumzika ndani ya saa 72 lakini Bodi ya ligi inatoa maelezo mengi kitu ambacho si sawa''.

Aidha Manara aliweka wazi kuwa Yanga ambayo ilikuwa na viporo 9 ilikuwa inapanga matokeo kwa kutumia mfumo wa 'Indirect' kwani kuna baadhi ya timu ambazo zilikuwa zinakaribia kushuka daraja huenda zisingekuwa na ushindani wakati ambao zitacheza na Yanga.

Hata hivyo kwa upande wa pili ambao ni Yanga na Azam FC msimu huu wao wapo kimya na hawajalalamika licha ya Simba kupumzika kwa zaidi ya saa 72 lakini imekuwa haichezi mechi zake za ligi na kuendelea na maandalizi ya michuano ya kimataifa.

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine