Monday , 22nd Feb , 2016

Uongozi wa klabu ya Yanga ya jijini Dar es salaam, umepongeza wachezaji, benchi la ufundi na kocha wa timu hiyo Hans Van Plujm kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Simba katika mchezo wa ligi kuu Tanzania bara uliopigwa Jumamosi Julai 20 mwaka huu.

Taarifa iliyotolewa na msemaji wa klabu hiyo Jerry Muro kwa niaba ya uongozi mzima wa Yanga, imesema uongozi unathamini juhudi za wachezaji hadi kupata mabao hayo mawili kwa bila, kwenye mchezo huo.

Taarifa hiyo imesema uongozi utaenzi jitihada hizo kwa kuwa ni mafanikio ya klabu na wanachama wa klabu hiyo wanatakiwa kujua thamani ya wachezaji kutoka kwa uongozi huo.

Aidha kwa upande mwingine,kikosi cha Yanga kimeanza mazoezi hii leo kwenye uwanja wa chuo cha polisi kurasini jijini Dar es Salaam na kesho kikosi hicho kitaingia kambini rasmi kujiandaa na mchezo wa kombe la FA dhidi ya JKT Mlale Jumatano Februari 24 mwaka huu uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.