Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Yanga yazidi kuijaza Simba 'presha' VPL

Tuesday , 17th Jan , 2017

Mabingwa watetezi wa ligi kuu Tanzania Bara, Yanga imezidi kuwafanya wapenzi wa Simba kuishi kwa wasiwasi baada ya leo kuchukua point 3 kwa Majimaji ya Songea, na kufikisha point 43, ikiwa ni point moja tu nyuma vinara wa ligi, Simba SC.

Yanga na Majimaji (Maktaba)

Katika mchezo wa leo, Yanga imetumia uzoefu na ukubwa wake katika ligi hiyo, ha kufanikiwa kupata bao pekee katika dakika ya 14 kupitia kwa Deus Kaseke aliyemalizia mpira uliopanguliwa na kipa wa Majimaji wakati akicheza kros ya Haruna Niyonzima kutoka winga ya kushoto.

Majimaji ambao wako chini ya udhamini mpya na kocha Kally Ongala, katika mchezo wa leo wameonesha mchezo wa ushindani huku wakimiliki mpira zaidi ya Yanga, lakini wamekosa mbinu ambazo zingeweza kuleta madhara kwenye lango la Yanga.

Hadi mwisho wa mchezo kutoka katika dimba la Majimaji Songea, Yanga bao 1, Majimaji 0.

Matokeo haya yanaiongezea Yanga mtaji wa kusaka kukaa kileleni kwani endapo Simba watashindwa kupata point 3 katika mcheo wa kesho,tofauti itakuwa ni point moja, ambayo itawafanya wawe na nafasi nzuri ya kuwashusha Simba kileleni.

Kwa upande wao Simba wanashuka dimbani kesho kukipiga na Mtibwa Sugar katika dimba la Jamhuri Morogoro.

HABARI ZAIDI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali