Katika mpambano huo wa raundi 10 mabondia hao walionyesha uwezo mkubwa hasa Mashali ambaye alionekana katika raundi za 6 za awali kwamba angeibuka na ushindi wa Knock out lakini hali ikabadilika katika raundi ya 7 baada ya Kaseba naye kuzinduka na kumshambulia Mashali
Na baada ya hapo zikapigwa raundi tatu za mwisho ambazo hazikuwa na mabadiliko makubwa kwani mabondia hao walikua wakishambuliana kwa zamu na baada ya mpambano huo nilizungumza na Bondia Thomas Mashali ambaye awali alitamba kummaliza mpinzani wake katika raundi nne za awali
Naye Japhet Kaseba ambaye watu wengi hawakutegemea kumaliza raundi zote 10 katika mpambano huo amesema uzoefu wa mchezo huo ndio umemfanya asiibuke na ushindi kwani yeye awali alikua akicheza kick boxing na amekubali matokeo hayo.