Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mzee ambaye hajawahi kula, kunywa kwa miaka 70

Friday , 6th Sep , 2019

Kuna mambo ukiambiwa unaweza usiamini sababu ni tofauti kabisa na namna unavyofahamu wewe au ilivyokawaida.

Prahlad Jani

Nchini India kuna mzee ambaye unaambiwa hajawahi kula wala kunywa maji kwa zaidi ya miaka 70.

Pengine ni jambo kubwa sana la kushangaza, inakuaje mtu hajala wala kunywa kwa miaka yote hiyo, wakati inafahamika kuwa kwa binadamu wa kawaida kama atakosa chakula na maji ndani ya siku tatu anaweza kufa.

Mzee Prahlad Jani amezaliwa mwaka 1929 na anasema hajawahi kugusa kitu chochote tangu mwaka 1940 mpaka sasa.

INAKUAJE MPAKA SASA YUPO HAI?

Kwa maelezo yake mwenyewe Prahlad anasema anapata nguvu kutoka kwa Mungu wake anayefahamika kwa jina la Amba' ambaye ndiye aliyempa muujiza huo na pale anapokuwa anasikia njaa kuna tundu dogo katika mdomo wake juu karibu na matundu ya pua, tundu hilo humpatia kitu kama mate mate yanayomfanya asisikie kutumia kitu chochote kile pale anaposikia njaa.

Mwaka 2003 alifanyiwa vipimo na madaktari ili kugundua ukweli wa jambo hilo kwa siku 10, madaktari wanasema kuwa katika siku hizo hawakuwahi kumuona akipata chakula au kunywa maji na uchunguzi wa mwili wake ulionesha uko vizuri kama mtu wa kawaida.

Haja ndogo yake ilionesha kutengenezwa katika kibofu lakini ilikuwa ikifyonzwa na mwili wake, jambo ambalo sio kawaida na kingine walichoona zaidi ni tundu dogo ndani ya mdomo juu kidogo karibu na matundu ya pua.

Mwaka 2010 utafiti mwingine tena ulifanyika na majibu waliyopata yalikua ni hayo hayo, mzee Prahlad hawakuwahi kumuona kwenda chooni au kula chochote.

Vyanzo: Lightdocumentary.com, Wikiversity.org

HABARI ZAIDI

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari

Picha ya Diddy na Cassie enzi za mahusiano yake

Diddy aomba msamaha kumshambulia EX wake Cassie

Rais wa Iran Ebrahim Raisi

Rais wa Iran afariki kwa ajali ya Helikopta

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu