Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ronaldo awatafuta wasichana waliomsaidia utotoni

Thursday , 19th Sep , 2019

Nyota wa klabu ya Juventus, Cristiano Ronaldo amezungumzia historia ya ndani ya maisha yake kipindi alipokuwa anaanza kucheza soka nchini Ureno. 

Cristiano Ronaldo

Akizungumza na ITV Football, Ronaldo amesema kuwa alipokuwa na miaka 10 au 11 mjini Lisbon nchini Ureno, hakuwa na pesa za kumuwezesha kuishi na alikuwa akiishi sehemu moja na wachezaji wenzake katika kambi.

Katika kipindi hicho alipokuwa kambini Jijini Lisbon, wazazi wake walikuwa wakiishi mjini Madeira na alikuwa akiwatembelea kila baada ya miezi mitatu kutokana na hali ya maisha ya wazazi wake kutokuwa nzuri.

"Ilikuwa ni kipindi kigumu sana kutokuwa karibu na wazazi. Tukiwa kambini, majira ya usiku wa saa 4:30 au saa 5 tulikukuwa tukihisi njaa, kwahiyo tulikuwa tukielekea katika mgahawa mmoja karibu na uwanja wetu ambapo tulikuwa tukienda kugonga mlango na kuuliza kama chakula kimebakia", amesimulia Ronaldo.

"Edna na wasichana wengine wawili walikuwa wakarimu kupitiliza, sikuweza kuwaona tena wale wasichana. Ninajaribu kuongea na watu mbalimbali nchini Ureno ili kufahamu walipo na nina imani kupitia majohiano haya, itasaidia kuwapata", ameongeza.

Ronaldo amesisitiza kuwa anataka kukutana na wasichana hao ili aweze kuwarudishia kitu kutokana na mafanikio yake hivi sasa. Anataka kuwaalika nyumbani kwake wapate chakula pamoja. 

Aidha katika majohiano hayo ambayo mwenyewe amesema ndiyo ya kwanza kwake kumtoa chozi, Ronaldo amezungumzia jinsi anavyomkumbuka baba yake ambaye amefariki dunia, akisema kuwa anatamani baba yake angekuwepo kipindi hiki ashuhudie mafanikio aliyo nayo pamoja na tuzo mbalimbali anazozipata.

 

HABARI ZAIDI

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90