Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ufafanuzi wa Simba kuhusu kuwasimamisha mastaa

Wednesday , 9th Oct , 2019

Uongozi wa klabu ya Simba umefafanua juu ya tetesi za wachezaji wake Jonas Mkude, Gadiel Michael, Erasto Nyoni na Clatous Chama zilizodai kuwa wachezaji hao wamesimamishwa.

Chama, Nyoni, Gadiel

Kupitia taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Mtendaji Mkuu wa Klabu hiyo, Simba ilifanya kikao cha ndani cha nidhamu mnamo Alhamisi, Oktoba 3 kujadili masuala ya kinidhamu pamoja na wachezaji hao kuhusu tuhuma za kutohudhuria mechi za kanda ya ziwa.

Klabu imesema kuwa kikao hicho kiliendeshwa kwa usawa na haki, ambapo walalamikiwa walitakiwa kujieleza na mashahidi waliitwa kutoa ushahidi kuhusiana na suala hilo.

Imesema suala hilo litamalizwa ndani ya klabu na kwamba kinachosubiriwa ni ripoti kutoka kwa kamati huru iliyoundwa na wanasheria wanne kuhakikisha kuwa haki inatendeka.

"Klabu ya Simba inasubiri wachezaji hao wamalize majukumu yao ya timu ya taifa kisha kukutana nao ili kulimaliza sakata hili, tofauti na taaria za uongo zilizotolewa kwenye baadhi ya vyombo vya habari mbalimbali kwamba wachezaji hao wamesimamishwa kwa kipindi cha mwezi mmoja kufanya shughuli zozote za klabu", imesema sehemu ya taarifa hiyo.

 

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine