Rais Magufuli ametoa kauli hiyo mkoani Lindi, wakati akihutubia kwenye kilele cha Mbio za Mwenge nchini, iliyoendana sambamba na kumbukumbu ya miaka 20 ya kifo cha Mwalimu Nyerere.
"Wote mnakumbuka Mwalimu Nyerere alikuwa hapendi rushwa, na yeyote ambaye alijihusisha na vitendo vya rushwa alipigwa bakora kabla ya kutoka na baada ya kutoka jela, kupitia hotuba zake nadhani mnajua hili."amesema Rais Magufuli
"Naikabidhi hii ripoti kwa TAKUKURU ukaikague, uiangalie wale wanaotakiwa kupelekwa mahakamani na wale ambao unaona huwawezi niletee ripoti zao, nataka Tanzania inyooke." amesema Rais Magufuli
Aidha Rais Magufuli amesema Serikali yake imemkumbuka kwa kutekeleza masuala mbalimbali ikiwemo kujenga viwanda, kutoa elimu bure.